Wakrito
 nchini na watanzania wametakiwa kuliombea taifa ili liweze kuvuka 
salama kipindi hiki kigumu chenye matukio makubwa ya upatikanaji wa 
katiba mpya pamoja na uchaguzi mkuu huku viongozi wakitakiwa kutenda 
haki kwani amani ni tunda la haki.
 
 
Askofu wa kanisa la AICT dayosisi ya Pwani Charles Salalah ametoa 
wito huo wakati wa ibada ya ijumaa kuu ambayo kitaifa imefanyika katika 
kanisa la AICT magomeni jijini Dar es Salaam ambapo amesema maeneo yote 
duniani ambayo yamekumbwa na machafuko chanzo kikubwa ni ukosefu wa haki
 hivyo ni wajibu wa kila kiongozi mwenye dhamana kutenda haki.
Ibada hiyo imehudhuriwa na wachungaji kutoka madhehebu mbalimbali 
ambayo pia imetumika kuliombea taifa pamoja na viongozi mbalimbali 
akiwemo rais Jakaya Kikwete ili mungu amjalie afya njema aweze 
kuliongoza taifa vyema sala iliyoongozwa na mchungaji Daniel Ntebi.
Katika kanisa la KKKT Azania Front ibada ya pasaka imefanyika na 
kupambwa na maigizo yaliyokuwa yanaonyesha mapito aliyopitia bwana yesu 
kristo hadi alipokufa msalabani ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kifo 
chake huku waziri mkuu mstaafu Mh Edward Lowassa ambaye amehudhuria 
ibada hiyo akizungumzia siku hii.
