LEO KATIKA HISTORIA: Aprili 4


McDonald Mariga Wanyama

1987: McDonald Mariga azaliwa
Mariga Wanyama ni mwanasoka wa aliyeweka rekodi ya kuwa raia wa kwanza kutoka nchini Kenya kucheza Ligi ya Mabingwa barani Ulaya. Rekodi hiyo aliiweka Machi 16, 2010 akiwa na klabu ya Inter Milan. Alizaliwa jijini Nairobi akianza soka lake Ulinzi Stars kabla ya kusajiliwa Tusker FC na baadaye Kenya Pipeline. Sasa anacheza soka nchini Italia akiwa na Parma.
1987: Sami Khedira azaliwa
Sami Khedira ni mchezaji wa soka kutoka nchini Ujerumani anayeitumikia klabu ya Real Madrid katika nafasi ya kiungo mkabaji. Alizaliwa mjini Stuttgart. Mwaka 2010 alitua Los Blancos akitokea VfB Stuggart alikoanzia soka lake. Hadi sasa anawaniwa na vilabu vya soka vya England kutaka saini yake mwishoni mwa msimu. 
2012: Dubravko Pavličić afariki dunia
Pavličić alikuwa mlinzi wa kati wa timu ya taifa ya Croatia na klabu ya Hércules (Hispania). Dubravko  anakumbukwa nchini Hispania kwani mwaka 1994 aliweka rekodi ya kuifunga Barcelona nyumbani na ugenini wakishinda 3-2 Nou Camp na baadaye 2-1 José Rico Pérez. Alizaliwa Novemba 28, 1967. Alifariki kwa kansa ya kongosho mjini Elche akiwa na umri wa miaka 44.

Post a Comment

http://www.princetarique.blogspot.com

أحدث أقدم

Comments System

blogger/disqus/facebook

Disqus Shortname

designcart