Nyota wa klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo anaweza kukumbwa na 
adhabu kutokana na ushangiliaji wake aliouonesha siku ya jumapili 
alipofunga goli dhidi ya mahasimu wao wa jadi Barcelona.
Siyo mara ya kwanza Ronaldo kufunga goli kwenye uwanja wa Nou Camp 
lakini siku ya jumapili baada ya kufunga alionesha kitendo ambacho 
mashabiki wa Barcelona wamedai kuwa alikuwa alikuwa anawatukana.
Mashabiki wamesema siyo mara ya kwanza kwa nahodha huyo wa Ureno 
kuonesha kitendo hicho bali imekuwa kawaida yake ya kuwatukana mashabiki
 wa upande wa upinzani wakati anapofunga goli, kitendo kama hicho 
kilitokea kwenye mchezo wa fainali wa ligi ya mabingwa ulaya msimu 
uliopita dhidi ya Atletico mchezaji huyo alivua shati na kuwarushia 
mashabiki wa upande wa pili.
Rais wa ligi ya Hispania  amesema  huwa wanakuwa makini kufatilia ishara
 ambazo uoneshwa na wachezaji wanapofunga magoli au pindi mchezo 
unapokuwa unaendelea kwahiyo bado wanafatilia na kama itagundulika kuwa 
alifanya kosa hilo basi mchezaji huyo atawajibishwa
