|  | 
| 
Mikel Arteta | 
1982: Mikel Arteta azaliwa
Huyu ni 
nahodha wa klabu ya Arsenal(England) akiweka rekodi ya kutoichezea timu 
ya taifa ya Hispania (La Roja) alizaliwa Donostia, San Sebastian. 
Alianza soka lake na FC Barcelona, baadaye akatolewa kwa mkopo PSG. 
Amewahi kuichezea Rangers ya Uskochi msimu wa 2002-03 wakitwaa mataji 
matatu kwa pamoja. Pia Real Sociedad ambako hakukaa sana. Msimu wa 
2004-05 alitolewa kwa mkopo Everton. Mwaka 2011 alisajiliwa na ‘Washika 
Bunduki’ wa London na Agosti 2014 aliteuliwa kuwa nahodha wa timu hiyo.
1974: George Foreman amtandika Ken Norton TKO
Bondia wa 
zamani nchini Marekani George Foreman ambaye alitwaa medali ya dhahabu 
katika Michuano  ya Olimpiki ya mwaka 1968 nchini Mexico alimzabua Ken 
Norton kwa TKO, kabla ya kupoteza dhidi ya Joe Frazier. Pia alipigwa na 
Muhammad Ali katika ‘Rumble in the Jungle’. Kabla hajastaafu alishinda 
mapambano 76 na kupoteza 5. Jarida la ‘The Ring’ limemuweka nafasi ya 9 
katika orodha ya watupa mawe wa zama zote. 
1992: Mike Tyson ahukumiwa miaka 10 jela
Mkali huyu 
aliyeweka rekodi ya kutetea taji lake mara 9 likiwemo pambano dhidi ya 
Larry Holmes na Frank Bruno, alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela baada
 ya kumbaka mwanadada mrembo Desiree Washington. Mwaka 1990 alipoteza 
taji lake dhidi ya James ‘Buster’ Douglas kwa KO katika raundi ya 10. 
Hata hivyo mwaka 1991 alifanikiwa kumchapa Donovan Ruddock mara mbili. 
Tyson ameshinda mapambano 50 akipoteza 6 na mawili alipewa ushindi wa 
mezani.
