Droo ya mashindano ya CHAN kufanyika April 5

Uwanja wa taifa wa Rwanda
Uwanja wa taifa wa Rwanda
Droo ya kombe la shirikisho Barani Afrika (CHAN) itafanyika tarehe 5 mwezi ujao kwenye makao makuu ya shirikisho la mpira Afrika yaliyoko jijini Cairo nchini Misri.
Jumla ya timu 42 zitapangwa kwenye makundi kulingana na kanda zinapotoka na kila kundi litakuwa linatoa timu tatu.
Timu hizo zitacheza raundi mbili isipokuwa nchi za Libya, morocco pamoja na Tunisia ambazo zitacheza zenyewe na kutoa timu mbili zitakazoshiriki fainali hizo.
Kanda ya A Magharibi itakuwa na timu za Gambia, Guinea, Guinea Bissau, Liberia, Mali, Mauritania, Senegal and Sierra Leone
Kanda ya Magharibi B itakuwa na makundi mawili ambapo kundi la kwanza litakuwa na timu za Burkina Faso, Côte d’Ivoire, Ghana, Niger, Nigeria and Togo huku kundi la pili likiwa na  timu za Cameroon, Central African Republic, Congo, Chad, DR Congo and Gabon
Kanda ya mashariki itakuwa na timu ya Rwanda ambaye ni mwenyeji, Burundi, Djibouti, Ethiopia, Kenya, Sudan, Tanzania and Uganda lakini timu ya Rwanda aihitaji kufuzu maana wao wana nafasi ya uwenyeji.
Kanda ya kusini itakuwa na timu za Angola, Botswana, Comoros, Mauritius, Lesotho, Mozambique, Namibia, Seychelles, South Africa, Swaziland, Zambia and Zimbabwe
Mechi za kufuzu zitaanza mwezi wa sita hadi mwezi wa nane mwaka huu ambapo  timu 15 zitaungana na mwenyeji Rwanda kushiriki michuano hiyo ambayo itafanyika mwezi wa kwanza mwaka ujao.
Kwasasa timu ambayo imeshikiria ubingwa huo ni timu ya taifa ya Libya.

Post a Comment

http://www.princetarique.blogspot.com

أحدث أقدم

Comments System

blogger/disqus/facebook

Disqus Shortname

designcart