Reli mpya ya mizigo kujengwa kuanzia DSM mpaka KIGOMA

Waziri wa uchukuzi SAMUEL SITTA
Waziri wa uchukuzi SAMUEL SITTA amesema serikali inaendelea na mchakato wa kujenga reli mpya itakayokua na urefu wa kilomita 2,561 itakayoanzia Jijini DSM hadi mkoani KIGOMA kwa kupitia katika miji kadhaa ambayo itagharibu Shilingi Trilioni kumi na nne, ndani ya miaka Miaka ijayo.

SITTA ametoa kauli hiyo jijini DSM katika mkutano na waandishi wa habari, ambapo amesema tayari kampuni ya Usimamizi wa Rasilimali za Reli – RAHCO imekamilisha utaratibu wa kumpata mshauri wa mradi huo.

Waziri SITTA ameongeza kuwa katika mradi huo serikali haitatoa fedha yoyote, ambapo mradi utagharamiwa na benki ambazo zitatoa fedha kama mkopo ambao utarejeshwa kutokana na makubaliano yatakayotokana na tozo ya mizigo itakayopitishwa katika reli hiyo.

Reli hiyo mpya ya kutoka DSM hadi mkoani KIGOMA itapita katika miji ya TABORA, MWANZA, ISAKA hadi RUSUMO, KAILUA – MPANDA – KAREMA na UVINZA hadi MUSINGATI nchini BURUNDI.

Post a Comment

http://www.princetarique.blogspot.com

Previous Post Next Post

Comments System

blogger/disqus/facebook

Disqus Shortname

designcart