Wafugaji washtakiwa kwa kuua simba 2 Kenya

 
Wafugaji washtakiwa kwa kuua simba 2 Kenya
Wafugaji wawili wa mifugo wamefikishwa mahakamani nchi Kenya.
Wanatuhumiwa kwa kuweka sumu kwenye mzoga wa ng'ombe ambao wafugaji hao wanadai kundi la simba liliwavamia na kuwaua.
Kundi la simba hao wanane linalofahamika kama The Marsh Pride lilionekana mwisho karibu na hoteli ya kifahari ya Governors Camp.
Wawili hao, Simindei Naururi na Kulangash Toposat wanakabiliwa na mashtaka ya kuua kwa kukusudia simba hao ambao ni rasli mali ya taifa.
Simba wanane wamegonjeka.
Simba hao ni maarufu baada yao kuonyeshwa katika makala ya wanyama pori ya runinga ya BBC ya Big Cat Diary.
 
Vifo hivyo ni kilele cha mzozo kati ya jamii ya wafugaji wa kuhama hama ya wa-Maasai ambao wanalazimika kuchunga mifugo wao ndani ya mbuga ya wanyama ya Maasai Mara
Vifo hivyo ni kilele cha mzozo kati ya jamii ya wafugaji wa kuhama hama ya wa-Maasai ambao wanalazimika kuchunga mifugo wao ndani ya mbuga ya wanyama ya Maasai Mara
Shirika la huduma ya wanyama pori nchini Kenya KWS limeonya huenda simba zaidi walikula mzoga huo wa ng'ombe uliowekwa sumu.
Wafugaji hao wanadai kuwa walivamiwa na kundi la Simba ambao waliua mifugo watatu.
Tukio hilo lilitokea jumamosi tarehe 5.Kufikia Jana simba wawili walikuwa wameaga dunia tayari.

Post a Comment

http://www.princetarique.blogspot.com

Previous Post Next Post

Comments System

blogger/disqus/facebook

Disqus Shortname

designcart