Miradi 2 utunzaji mazingira yazinduliwa wilayani MAKETE


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira, Dr BINILITH MAHENGE
 
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, anayeshughulikia Mazingira, Dr BINILITH MAHENGE amezindua miradi mikubwa miwili ya utunzaji na Uhifadhi wa Mazingira itakayoanza kutekelezwa katika wilaya Mbili nchini, wilaya ya Makete na wilaya ya Iringa Vijijini, kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo duniani-UNDP kwa kushirikiana na Shirika lisilokuwa la kiserikali linalotoa elimu juu ya mazingira kwa watoto –CCDO.

Waziri MAHENGE amezindua miradi hiyo sambamba na uzinduzi wa mwongozo wa kufundishia somo la Mazingira kwa wanafunzi wa shule za Msingi.

Miradi hiyo ni pamoja na mradi wa kuiwezesha jamii kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi, na Mradi wa upandaji wa miti ili kuboresha hifadhi ya misitu iliyoharibiwa na watu wasiojulikana kuzunguka wilaya za Iringa Vijijini na Makete, mkoani Njombe.

Aidha idadi ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali mengi yamekuwa yakipata msaada wa fedha za wahisani ili kuwasaidia wananchi kujua mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira, lakini baadhi ya viongozi wa mashirika hayo wamekuwa wakijinufaisha wao wenyewe.

Post a Comment

http://www.princetarique.blogspot.com

Previous Post Next Post

Comments System

blogger/disqus/facebook

Disqus Shortname

designcart