Ni
mwaka wenye hadhi na uzito kwa mcheza tennis Andy Murray, hali hiyo si
tu kutokana na matumaini yake ya kuongeza taji la pili la Grand Slam
bali ni mpango alionao wa kufunga ndoa na mpenzi wake Kim Sears April
mwaka huu.
Mchezaji huyo raia wa Scotland amerejea katika nafasi
ya nne duniani baada ya awali kuporomoka kutokana na upasuaji wa mgongo
aliofanyiwa.Furaha ya mchezaji huyo inachagizwa zaidi kutokana na rekodi mpya aliyojiwekea baada ya kufanikiwa kutinga nusu fainali katika mashindano ya Indian Wells yanayoendelea huko California Marekani.