Wana
 wawili wa aliyekuwa Rais wa Misri Hosni Mubarak wameachiliwa kutoka 
jela, miaka minne baada ya kukamatwa na kuzuiliwa kwa pamoja na baba 
yao.>>>>>
Wakuu wa gereza wanasema kuwa Gamal na Alaa Mubarak wote wanabiashara maarufu waliachiliwa mapema leo Jumatatu.Mubarak anaendelea kuzuiliwa katika Hospitali moja ya kijeshi, ambapo anatumikia hukumu ya matumizi mabaya ya pesa za umma.
